Saturday 23 June 2012

MADAKTARI ACHENI KAZI SERIKALINI

Kugoma sio dawa ya tatizo.Dawa ni kuacha kazi ya kutumwa na serikali na kuungana kuanzisha Hospitali yenu itakayokizi mahitaji na iliyo bora.

Wengi wenu ni madaktari bingwa kwa nini msiombe mikopo mikubwa na kujiajili wenyewe kwa kuanzisha hospital yenu na kujilipa mishahara mikubwa..

Mkiwa na hospitali yenu mtanunua vifaa vya kisasa na wananchi watakuja kwenu na hata hao wanaotibiwa nje ya nchi pia watavutiwa na huduma zenu ziliboreshwa vzr.

Rejeeni kazini na mjipange upya.kuweni na mikakati endelevu kama wenzenu wa nchi nyengine ..

Wajulisheni wananchi mmeacha kazi ili muanzishe hospitali yenu yenye kiwango mtakacho lizika nacho.

Kimtazamo hamuigomei serikali mnamgomea yule raia alie lala na kulalama kwa maumivu uku ndugu yake akimuangalia akiteseka hadi kumfia mkononi mwake wakiwa wanaangaliana hali ameishaiaga dunia..

No comments:

Post a Comment

Angalia unapoandika usije kuleta machafuko
na hali ya sinto fahamu